Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Hamis Mkunga (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Usimamizi na Payrol, Jeanfrida Mushumbusi (kulia) wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma yaliyofanyika kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.