Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii ambaye ni Afisa Ustawi wa Jamii Mkuu, Bi. Herieth Mpili akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Dkt. Charles Kato kuzungumza na Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakati wa semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.