Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ngolela, Bw. Samsoni Anyosisye (wanne kutoka kushoto) akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (wa kwanza kutoka kulia) wakati wa ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Shule ya msingi Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya
Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya watumishi wa umma wa Shule ya msingi Ngolela, iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoa wa Mbeya
Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watumishi Housing Investment (WHI) ikiwa katika picha ya pamoja na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ngolela, Bw. Samsoni Anyosisye (wanne kutoka kushoto) mara baada ya timu hiyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Shule ya msingi Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya
Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (aliyenyoosha mkono) akitaka ufafanuzi wa jambo wakati wa ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Shule ya msingi Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mipango na Bajeti,Bi Julieth Magambo wa Ofisi hiyo.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akizungumza jambo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi kwa watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia mada kuhusu Itifaki wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia mada kuhusu Itifaki wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia mada kuhusu Itifaki wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Mtumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Joyce Atanas akiuliza swali kuhusu Itifaki mara baada ya Mhadhiri wa Diplomasia, Bw. Lucas Humo (hayupo pichani) kuwasilisha mada kuhusu Itifaki mbalimbali katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo kwa watumishi wa ofisi hiyo yaliyolenga kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Mtumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Joyce Atanas akiuliza swali kuhusu Itifaki mara baada ya Mhadhiri wa Diplomasia, Bw. Lucas Humo (hayupo pichani) kuwasilisha mada kuhusu Itifaki mbalimbali katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo kwa watumishi wa ofisi hiyo yaliyolenga kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.