Mwakilishi wa Katibu Mkuu-UTUMISHI, SACP Ibrahimu Mahumi akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) kuzungumza na Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na Wananchi wa Mkoa wa Tanga mara baada ya Waziri huyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.