Habari
WAZIRI SIMBACHAWENE AITAKA TASAF KUWA SHIRIKISHI ILI KUWAGUSA WALENGWA HALISI WA UMASIKINI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao. Wa pili kulia waliokaa ni Naibu Waziri wake, Mhe. Ridhiwani Kikwete na wa pili kushoto waliokaa ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Bw. Shedrack Mziray.