Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Habari

WAZIRI JENISTA AKUTANA NA BALOZI WA INDIA NCHINI TANZANIA NA KUFANYA MAZUNGUMZO YA KUENDELEZA USHIRIKIANO KATIKA KUWAJENGEA UWEZO WATUMISHI WA UMMA, MATUMIZI YA TEHAMA SERIKALINI NA UWEZESHAJI WA KAYA MASKINI


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na Balozi wa India nchini Tanzania, Mhe. Binaya Pradhan (hayupo pichani) alipokutana naye jijini Dar es Salaam na kufanya mazungumzo ya kuendeleza ushirikiano katika kuwajengea uwezo watumishi wa umma, matumizi ya TEHAMA serikalini na uwezeshaji wa kaya maskini.