Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Habari

WANAWAKE WA OFISI YA RAIS, UTUMISHI NA UTAWALA BORA  WAUNGANA NA WANAWAKE WENGINE MKOANI DODOMA  KUADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI


Watumishi Wanawake  wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora  wameungana  na wanawake wengine  jijini Dodoma na Duniani kote  kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani  ambayo huadhimishwa Machi  08 kila mwaka.

Watumishi hao wameongozwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Ofisi hiyo,   sehemu ya Utawala, Bi Mwalibora Mwamtuya katika kuadhimisha Siku hiyo iliyofanyika katika viwanja vya Chinangali kwa ngazi ya Mkoa,  jijini Dodoma.

Maadhimisho hayo Kitaifa yamefanyika  Jijini Arusha  ambapo Mgeni Rasmi alikuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kauli mbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu ni  ‘’ Wanawake  na Wasichana 2025: Tuimarishe  Haki, Usawa na Uwezeshaji" Lengo likiwa ni kuhamasisha jamii kukuza  Usawa, Haki na Uwezeshaji wa Wanawake  na Wasichana  kwa kuzingatia kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 ili wajiamini, wajiandae na wajitokeze kugombea nafasi za uongozi.