Habari
WANANCHI WASISITIZWA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KATIKA VITA DHIDI YA RUSHWA

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe.Hemed Suleiman Abdulla akiwa na baadhi ya viongozi pamoja na wananchi wakiwa kwenye matembezi ya hiari yanayofahamika kwa jina la 'Ant-Corruption Work' kwa lengo la kufikisha ujumbe ulimwenguni kuwa Bara la Afrika linapinga rushwa kabla ya kufungua Maadhimisho ya Siku ya Kupambana na Rushwa Barani Afrika.