Habari
WAAJIRIWA WAPYA 553 WA TAKUKURU WATAKIWA KUTUMIKIA MIAKA 5 BILA KUHAMIA TAASISI NYINGINE ILI KUTIMIZA LENGO LA MHE. RAIS LA KUTOKOMEZA RUSHWA NCHINI

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akishuhudia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakionyeshwa na wahitimu wa mafunzo ya Maafisa Uchunguzi na Wachunguzi Wasaidizi wapya wanaoajiriwa na TAKUKURU (hawapo pichani) kabla ya kufunga mafunzo hayo mjini Moshi. Kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Kamishna wa Polisi, Salum Hamduni na kushoto kwake ni Mkuu wa Chuo cha Polisi Tanzania SACP Ramadhani Mungi.