Habari
WAAJIRIWA WAPYA 553 WA TAKUKURU WATAKIWA KUTUMIKIA MIAKA 5 BILA KUHAMIA TAASISI NYINGINE ILI KUTIMIZA LENGO LA MHE. RAIS LA KUTOKOMEZA RUSHWA NCHINI

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akipokea heshima ya gwaride la wahitimu wa mafunzo ya Maafisa Uchunguzi na Wachunguzi Wasaidizi wapya wanaoajiriwa na TAKUKURU wakati akifunga mafunzo hayo mjini Moshi.