Habari
WAAJIRI WATAKIWA KUANDAA MADAWATI YA MSAADA ILI KUWEZESHA UTEKELEZAJI WA MAELEKEZO YA MHE. RAIS YA KUWAREJESHEA MICHANGO YAO WATUMISHI WA UMMA WALIOONDOLEWA KWA KUGHUSHI VYETI

Sehemu ya Waandishi wa Habari wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Mhe. Prof. Joyce Ndalichako (hawapo pichani) wakati wa mkutano vya vyombo vya habari leo jijini Dodoma kuhusu maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan la kuwarejeshea michango ya Mifuko ya Hifadhi za Jamii watumishi walioondolewa kwenye utumishi wa umma kwa kosa la kughushi vyeti.