Habari
VIONGOZI WANAWAKE WALIOHITIMU MAFUNZO YA UONGOZI WATAKIWA KUJIAMINI NA KUFANYA KAZI KWA UFANISI ILI KUWAHUDUMIA WANANCHI

Mwakilishi wa wahitimu wa programu ya mafunzo kwa viongozi wanawake Bi. Mwanaamani Mtoo, akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wenzie kabla ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuwatunuku vyeti wahitimu katika Mahafali ya Sita ya Taasisi ya UONGOZI yaliyofanyika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.