Habari
VIJANA 350 WANAOTARAJIWA KUAJIRIWA NA TAKUKURU WAASWA KUZINGATIA MAFUNZO YA UCHUNGUZI ILI KUOKOA FEDHA ZA UMMA ZINAZOPOTEA KUTOKANA NA UBADHIRIFU

Vijana wanaotarajiwa kuajiriwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) wakati akifungua mafunzo ya awali ya uchunguzi kwa vijana hao yanayofanyika katika Shule ya Polisi Moshi.