Habari
UANZISHWAJI WA MFUKO WA UWEKEZAJI WA PAMOJA WA ‘FAIDA FUND’ NI MATOKEO YA UTAWALA BORA WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na wadau jijini Dar es salaam wakati akizindua mauzo ya vipande vya mfuko wa uwekezaji wa pamoja wa FAIDA FUND ulioanzishwa na Watumishi Housing Investments (WHI) ili kuwawezesha Watanzania wenye kipato cha chini kupata mitaji itakayoboresha maisha yao.