Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Habari

TASAF YAGUSA MAISHA YA WANANCHI KIJIJI CHA KITANGA KWA KUWAJENGEA VISIMA VYA MAJI SAFI NA SALAMA


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akichota maji kwenye kisima kilichojengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwa ajili ya kuwahudumia wananchi mara baada ya kukagua kisima hicho katika Kijiji cha Kitanga wilayani Kisarawe mkoani Pwani.