Habari
SERIKALI KUPITIA TASAF YAJENGA BWENI KIJIJI CHA BUKUNDI KUONGEZA UFAULU WA WANAFUNZI NA KUWAEPUSHA NA MIMBA ZA UTOTONI

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi (Wakwanza kulia) akisikiliza taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa bweni la wanafunzi shule ya Sekondari Bukundi wilayani Meatu, wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua mradi wa ujenzi wa bweni la wanafunzi katika shule ya Sekondari Bukundi wilayani humo. Katikati ni Mkuu wa Wilaya Meatu, Mhe. Fauzia Ngatumbura na wakwanza kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu Mhe. Prisca Kayombo.