Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Habari

SERIKALI HAITOMVUMILIA KIONGOZI YEYOTE ATAKAYESHINDWA KUSIMAMIA VIZURI RASILIMALIWATU KWA USTAWI WA TAIFA


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana baadhi ya viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, mara baada ya kuwasili Wilayani humo ili kuzungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri hiyo, wakati ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi walio katika halmashauri hiyo.