Habari
SERIKALI HAITOMVUMILIA KIONGOZI YEYOTE ATAKAYESHINDWA KUSIMAMIA VIZURI RASILIMALIWATU KWA USTAWI WA TAIFA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akiimba Wimbo wa Taifa na viongozi wengine walio meza kuu kabla ya kuzungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro, wakati ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi katika halmashauri hiyo.