Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Habari

RAIS KAGAME AWASILI TANZANIA KUSHIRIKI MKUTANO WA  KUJADILI AMANI YA DRC


Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame amewasili nchini Tanzania kwa ajili ya mkutano wa kujadili amani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC),

Mhe. Kagame  amewasili asubuhi ya leo Jumamosi Februari 8, 2025 na kupokewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere

Mkutano huo unafanyika huku vikundi vya waasi chini ya Alliance Fleuve Congo (AFC/M23) vimekamata miji ya Goma, Kivu Kaskazini na Nyabibwe, Kivu Kusini vikielekea Bukavu.