Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Habari

OFISI YA RAIS-UTUMISHI YATEKELEZA MAELEKEZO YA MHE. RAIS YA KUHUISHA MIUNDO YA MAENDELEO YA UTUMISHI YA KADA ZA MAKATIBU MAHSUSI NA WATUNZA KUMBUKUBU NA NYARAKA ITAKAYOANZA KUTUMIKA MWEZI JULAI, 2023


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akitoa maelezo mafupi kwa    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu mkutano wa Makatibu Mahsusi na Watunza Kumbukumbu na Nyaraka wakati wa kilele cha Mafunzo ya Uadilifu kwa Wanachama wa Chama cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA) na Mkutano Mkuu wa 10 wa Chama cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA) uliofanyika Zanzibar.