Habari
OFISI YA RAIS-UTUMISHI YAPONGEZWA NA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA KWA KUIPA USHIRIKIANO KAMATI HIYO WAKATI WA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YAKE

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akitoa ufafanuzi wa moja ya hoja iliyowasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhusu Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo (TGFA, eGA na Taasisi ya UONGOZI) kwa Mwaka 2022/23.