Habari
OFISI YA RAIS-UTUMISHI KUSHIRIKIANA NA TUME YA HAKI ZA BINADAMU KUJENGA UTAMADUNI WA KUHESHIMU HAKI ZA BINADAMU, MISINGI YA UTAWALA BORA NA UTU WA MTU

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akiwa katika picha ya pamoja na Makamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, watendaji wa ofisi yake na wa tume hiyo waliofika ofisini kwake jijini Dodoma kwa lengo la kubadilishana uzoefu. Wa kwanza kulia kwake ni Mwenyekiti wa Tume, Jaji Mstaafu Mhe. Mathew Mwaimu na wa kwanza kushoto kwake ni Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi.