Habari
NAIBU WAZIRI KIKWETE AWATAKA MAAFISA UTUMISHI KUWA WABUNIFU KATIKA UTENDAJI KAZI KWA MAENDELEO YA TAIFA

Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mhe. Nickson Simon akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kuzungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili.