Habari
MWONGOZO WA KUDHIBITI VVU, UKIMWI NA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA WAHUISHWA KULINDA AFYA ZA WATUMISHI ILI WAWE NA TIJA KATIKA TAIFA

Mratibu wa Kinga na Mwitikio wa kitaifa dhidi ya VVU, Dkt. Hafidh Ameir akitoa taarifa ya hali ya VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza kabla ya kumkaribisha Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Agness Meena (hayupo pichani) kufungua kikao kazi cha kujadili Mwongozo wa Kudhibiti VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza mahali pa kazi kilichofanyika jijini Dodoma.