Habari
MHE. SIMBACHAWENE AWATAKA WAHITIMU WA TPSC KUFAHAMU KUWA UTUMISHI WA UMMA NI IBADA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akisindikiza maandamano ya wahitimu wa kozi mbalimbali katika mahafali ya 37 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika mkoani Tanga. Kushoto kwake ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi na kulia kwake ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Florens Turuka.