Habari
MHE. SIMBACHAWENE AIPONGEZA WHI KWA KUENDELEA KUJENGA MAKAZI BORA YA WATUMISHI , ASISITIZA KUJENGA ZAIDI KARIBU NA MAENEO YA KAZI

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuzungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kukagua mradi wa nyumba zilizojengwa na Watumishi Housing Investments (WHI) eneo la Njedengwa na Kisasa Relini jijini Dodoma wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa WHI.