Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Habari

MHE. SIMBACHAWENE ADHAMIRIA KUSIMAMIA WATUMISHI WA UMMA KUTUMIA VEMA SAA ZA KAZI KUWAHUDUMIA WANANCHI


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na watumishi wa ofisi yake alipowasili ofisini kwake Mtumba Jijini Dodoma, mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 02 Aprili, 2023 Ikulu Jijini Dar es Salaam kuwa waziri mwenye dhamana ya kusimamia Utumishi wa Umma na Utawala Bora nchini. Wa kwanza kulia ni Naibu Waziri wake Mhe. Ridhiwani Kikwete, Wa pili kutoka kushoto ni Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi na Wa kwanza kushoto na Naibu Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Xavier Daudi.