Habari
MHE. NDEJEMBI AKEMEA TABIA YA WAAJIRI SERIKALINI KUFICHA BARUA ZA UHAMISHO WA WATUMISHI WA UMMA ZILIZORIDHIWA NA MAMLAKA

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deogratius Ndejembi (katikati) akisikiliza hoja iliyokuwa ikiwasilishwa na mtumishi wa Manispaa ya Kigoma, wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma wa Halmashauri hiyo. Kushoto kwake ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma, Bw. Ntime Mwalyambi na kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mhe. Ester Mahawe.