Habari
MHE. KIKWETE AWAPONGEZA VIONGOZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BAGAMOYO KWA KUSIMAMIA NA KUWAHUDUMIA VIZURI WALENGWA WA TASAF

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Bw. Shauri Selenda akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kuzungumza na wanachi na walengwa wa TASAF wakati wa ziara yake ya kikazi katika Halmashauri hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF.