Habari
MHE. KIKWETE AWAPONGEZA VIONGOZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BAGAMOYO KWA KUSIMAMIA NA KUWAHUDUMIA VIZURI WALENGWA WA TASAF

Sehemu ya wananchi na walengwa wa TASAF wa Kata ya Dunda, Kijiji cha Dunda, Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati akizungumza nao alipokuwa kwenye ziara ya kikazi iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika halmashauri hiyo.