Habari
MHE. JENISTA NA MHE. KAIRUKI WAWEKA MKAKATI KUTEKELEZA MAELEKEZO YA MHE. RAIS YA KUIMARISHA MAADILI KATIKA UTUMISHI WA UMMA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Angellah Kairuki wakifuatilia taarifa ya mpango kazi iliyokuwa ikiwasilishwa na Watendaji wa Ofisi zao leo jijini Dodoma juu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ya kuboresha maadili katika utumishi wa umma.