Habari
MHE. JENISTA AWATAKA WATUMISHI WA OFISI YAKE KUTOA USHIRIKIANO WA KIUTENDAJI KWA VIONGOZI WAPYA ILI KUENDELEA KUUBORESHA UTUMISHI WA UMMA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akimkaribisha Katibu Mkuu wa ofisi yake Bw. Juma Mkomi mara baada ya kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma baada ya kuteuliwa na kuapishwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI. Nyuma ya Mhe. Waziri Jenista ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi.