Habari
MHE. JENISTA AWATAKA WATUMISHI WA OFISI YAKE KUTOA USHIRIKIANO WA KIUTENDAJI KWA VIONGOZI WAPYA ILI KUENDELEA KUUBORESHA UTUMISHI WA UMMA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama (meza kuu) akizungumza jambo na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (kushoto) mara baada ya Katibu Mkuu huyo kuripoti katika ofisi hizo Mtumba jijini Dodoma. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi.