Habari
MHE. JENISTA AWATAKA WATUMISHI WA OFISI YAKE KUTOA USHIRIKIANO WA KIUTENDAJI KWA VIONGOZI WAPYA ILI KUENDELEA KUUBORESHA UTUMISHI WA UMMA

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (wa pili kutoka kushoto) akipokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi yake kutoka kwa mtangulizi wake, Dkt. Laurean Ndumbaro (wa kwanza kulia) mara baada ya Bw. Mkomi kuripoti rasmi katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma. Wanaoshuhudia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete.