Habari
MHE. JENISTA ATOA WITO KWA WANANCHI KUSHIRIKIANA NA TAKUKURU KUZUIA VITENDO VYA RUSHWA KWENYE MIRADI YA MAENDELEO

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akitoa maelekezo ya ukamilishwaji wa miundombinu katika nyumba ya watumishi wa Zahanati ya Kijiji cha Ihayabuyaga, Halmashauri ya Wilaya ya Magu, mkoani Mwanza wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya TASAF wilayani humo.