Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Habari

MHE JENISTA ARIDHISHWA NA NAMNA e-GA INAVYOWAJENGEA UWEZO VIJANA WA VYUO VIKUU KUFANYA TAFITI NA UBUNIFU WA MIFUMO YA TEHAMA KATIKA KUTATUA CHANGAMOTO KWENYE SEKTA MBALIMBALI NCHINI


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya vijana wa Vyuo Vikuu wanaofanya utafiti na ubunifu wa mifumo ya TEHAMA kupitia Kituo cha Utafiti, Ubunifu na Uendelezaji wa Mifumo cha Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) mara baada ya kumaliza kikao kazi chake na vijana hao kilichofanyika jijini Dodoma. Wakwanza kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi na wakwanza kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) Mhandisi Benedict Ndomba.