Habari
MHE JENISTA ARIDHISHWA NA NAMNA e-GA INAVYOWAJENGEA UWEZO VIJANA WA VYUO VIKUU KUFANYA TAFITI NA UBUNIFU WA MIFUMO YA TEHAMA KATIKA KUTATUA CHANGAMOTO KWENYE SEKTA MBALIMBALI NCHINI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akizungumza wakati wa kikao kazi chake na vijana wa Vyuo Vikuu wanaofanya utafiti na ubunifu wa mifumo ya TEHAMA kupitia Kituo cha Utafiti, Ubunifu na Uendelezaji wa Mifumo cha Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kilichofanyika jijini Dodoma.