Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Habari

MHE. JENISTA AMUAGIZA MRATIBU WA TASAF HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA KUHAKIKISHA WOTE WANAOSTAHILI KUINGIZWA KWENYE MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI WANAANDIKISHWA


Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini na wananchi wa Kijiji cha Mtyangimbole, Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, mkoani Ruvuma wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika halmashauri hiyo.