Habari
MHE. JENISTA AIHIMIZA TGFA KUKAMILISHA UJENZI WA KARAKANA YA NDEGE JIJINI DAR ES SALAAM NA KUJIPANGA KWA UJENZI WA MAKAO MAKUU YA OFISI NA KARAKANA YA NDEGE JIJINI DODOMA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akisisitiza jambo kwenye Menejimenti ya Wakala ya Ndege za Serikali wakati wa kikao kazi chake na menejimenti hiyo jijini Dar es Salaam kilicholenga kuhimiza uwajibikaji. Kushoto kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Ndege za Serikali, Mhandisi John Nzulule na kulia kwake ni Mkurugenzi wa Sera na Mipango Ofisi ya Rais-Ikulu, Bibi Ened Munthali.