Habari
MFUKO WA UWEKEZAJI WA PAMOJA WA ‘FAIDA FUND’ UMELENGA KUWANUFAISHA WATANZANIA WA KIPATO CHA CHINI, KATI NA CHA JUU

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na wadau wa Watumishi Housing Investments (WHI) jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya uzinduzi wa mfuko wa uwekezaji wa pamoja wa FAIDA FUND ulioanzishwa na WHI kuwawezesha Watanzania kuwekeza kwenye mfuko huo ili kupata mtaji utakaoboresha maisha yao.