Habari
MAHITAJI YA MAFUNZO KWA WATUMISHI WA UMMA KUAINISHWA KWA KUZINGATIA MABADILIKO YA KIUTENDAJI, TEKNOLOJIA NA VIPAUMBELE VYA SERIKALI

Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais- UTUMISHI, Dkt. Edith Rwiza, akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bi. Leila Mavika (Wa kwanza kulia) kufungua kikao kazi cha kujadili maeneo muhimu yenye uhitaji wa mafunzo kwa watumishi wa umma kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mtumba jijini Dodoma.