Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Habari

MAHITAJI YA MAFUNZO KWA WATUMISHI WA UMMA KUAINISHWA KWA KUZINGATIA MABADILIKO YA KIUTENDAJI, TEKNOLOJIA NA VIPAUMBELE VYA SERIKALI


Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bi. Leila Mavika akizungumza na wadau kutoka katika taasisi za umma (hawapo pichani) wakati akifungua kikao kazi cha wadau hao kilicholenga kujadili maeneo muhimu yenye uhitaji wa mafunzo kwa watumishi wa umma, kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mtumba jijini Dodoma.