Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Habari

MAADHIMISHO YA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI (MEI MOSI)


Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, leo tarehe 1 Mei, 2026 wameungana na watumishi wengine kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) yenye kauli mbiu isemayo “Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050” ambapo kimkoa yamefanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.