Habari
LIKIZO KWA WATUMISHI WA UMMA NYAKATI ZA SIKUKUU ZISIWE KIKWAZO CHA KUWAHUDUMIA WANANCHI-Mhe. Ndejembi

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na watumishi wa Manispaa ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam (hawapo pichani), akiwa katika ziara yake ya kikazi yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma walio katika Wilaya hiyo.