Habari
KAMATI YA USEMI YAELEKEZA UMILIKI WA HATI MILIKI ZA ARDHI ZA FAMILIA UWE WA AKINA MAMA NA BABA

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Manyemba wilayani Chamwino, wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, iliyolenga kukagua utekelezaji wa shughuli za Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge (MKURABITA) wilayani humo.