Habari
KAMATI YA BUNGE YA UTAWALA YARIDHISHWA NA JITIHADA ZA MLENGWA WA TASAF WILAYANI UYUI NA KUMCHANGIA 530,000/= KUMUWEZESHA KUKAMILISHA UJENZI WA NYUMBA YA KUISHI

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa mchango kwa Mlengwa wa TASAF wa Kata ya Magiri wilayani Uyui, mkoani Tabora, Bi. Amina Abdallah ikiwa ni sehemu ya kuwaunga mkono Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Utawala, Katiba na Sheria, vingozi na watendaji wa Serikali waliomchangia mlengwa huyo ili kumuwezesha kukamilisha ujenzi wa nyumba aliyoianza kuijenga kutokana na ruzuku ya TASAF anayoipata.