Habari
FURSA ZA MAFUNZO KWA WATANZANIA NJE YA NCHI NI MATOKEO YA MAHUSIANO MAZURI YA KIDIPLOMASIA YANAYOJENGWA NA RAIS MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

Mmoja wa watumishi wa umma walionufaika na mafunzo nchini Korea yanayofadhiliwa na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Serikali ya Korea (KOICA) Bi. Maria Nkangali ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Mji Kibaha akielezea namna alivyonufaika na mafunzo mara baada ya watumishi hao kumtembelea Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama ofisini kwake jijini Dodoma.