Habari
DKT. NDUMBARO AELEKEZA MWONGOZO WA MPANGO WA URITHISHANAJI MADARAKA UBORESHWE KUENDANA NA DHAMIRA YA MHE. RAIS YA KUUJENGA UTUMISHI WA UMMA WENYE UADILIFU NA UWAJIBIKAJI

Sehemu ya wadau kutoka katika taasisi mbalimbali za umma wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi cha kujadili Mwongozo wa Mpango wa Urithishanaji Madaraka katika Utumishi wa Umma kilichofanyika ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.