Habari
WAAJIRI SERIKALINI WATAKIWA KUTOKWEPA JUKUMU LA KUWACHUKULIA HATUA WATUMISHI WANAOKIUKA MAADILI

Sehemu ya wadau wa usimamizi wa maadili katika utumishi wa umma wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) wakati akifunga kikao kazi cha siku mbili cha wadau hao kilicholenga kujadili matokeo ya tafiti ya hali ya uzingatiaji maadili katika utumishi wa umma ya mwaka 2022, jijini Dodoma.