Habari
SERIKALI IMETHIBITISHA KUJALI MASILAHI YA WATUMISHI KWA KUTUMIA SHILINGI BILIONI 50.7 KILA MWEZI KULIPA MISHAHARA MIPYA YA WATUMISHI 229,792 WALIOPANDISHWA MADARAJA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akisikiliza taarifa ya utekelezaji ya utumishi na utawala kwa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Ruvuma iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi hao.