Habari
RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AWAJENGEA SOKO LA KISASA WANANCHI WA PERAMIHO KUPITIA TASAF

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akikagua ujenzi wa soko la kisasa la Peramiho linalojengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma.