Habari
NYUMBA ZA WATUMISHI WA KITUO CHA AFYA NYABILEZI ZIMEJENGWA NA TASAF KUWAWEZESHA WATUMISHI KUTOA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

Mganga Mfawidhi wa kituo cha afya cha Nyabilezi (Nyabilezi Health Centre) Bi. Lucia Simbila (Wa kwanza kulia) akifafanua jambo kuhusu utendaji kazi wa kituo hicho kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini wilayani Chato mkoani Geita.