Tanzania emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Habari

MAKTABA YA UONGOZI KUCHOCHEA UWAJIBIKAJI WA VIONGOZI KATIKA KULITUMIKIA TAIFA - Mhe. Jenista


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na wadau wa Taasisi ya UONGOZI mara baada ya kuzindua rasmi maktaba ya Uongozi na toleo la Kiswahili la tawasifu ya Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa “Maisha Yangu, Kusudi Langu” katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.